Mafunzo ya matumizi sahihi ya viuatilifu na utunzaji wa mazingira kupitia mpango wa kuhimili Mifumo ya Chakula Tanzania (TFSRP).
BW. MAVIKA AIPONGEZA WIZARA YA KILIMO KWA KUPENDEKEZA ASA KATIKA UTEKELEZA WA PROGRAMU YA TFSRP
Na Mwandishi wetu- Morogoro
Kaimu Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Mbegu za Kilimo (ASA) Bw. Leo Mavika ameipongeza Wizara ya Kilimo kwa kuipendekeza (ASA) katika utekelezaji wa Programu ya Mifumo Himilivu ya Chakula Tanzania (TFSRP) .
Shukrani hizo zimetolewa Septemba 13, 2025 na Bw. Mavika wakati akifunga mafunzo ya Matumizi sahihi ya Viuwatilifu na utunzaji wa Mazingira kupitia Program ya Mifumo himilivu ya Chakula Tanzania (TFSRP).
Bw. Mavika amesema, mafunzo hayo ni muhimu kwetu ili kuongeza uzalishaji wenye tija na kutunza mazingira.
"Mafunzo haya yatawajengea uwezo wa kufanya Matumizi sahihi ya Viuwatilifu na utunzaji wa Mazingira mashambani, hii itachochea mazingira rafiki ya uzalishaji wa mbegu bora za kilimo na tija" amesema Bw. Mavika
“Naishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya Rais wa awamu ya sita Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kutoa fedha kwa ajili ya Sekta ya Kilimo” amesema Bw. Mavika
Aidha amempongeza Waziri wa Kilimo Mhe. Hussein Bashe (Mb) na Menejimenti ya Wizara ya kilimo kwa kuipambania Sekta ya kilimo na kuleta mageuzi makubwa ya Kilimo hapa nchini kwa kusimamia vema upatikanaji wa fedha kwa ajili ya programu hii na shughuli mbalimbali za kilimo ikiwa ni pamoja na kuipendekeza ASA katika utekelezaji wa Mradi huu wa TFSRP.
