Mafunzo ya matumizi sahihi ya viuatilifu na utunzaji wa mazingira kupitia mpango wa kuhimili Mifumo ya Chakula Tanzania (TFSRP).
13 Sep, 2025
Mafunzo ya matumizi sahihi ya viuatilifu na utunzaji wa mazingira kupitia mpango wa kuhimili Mifumo ya Chakula Tanzania (TFSRP).

BW. MAVIKA  AIPONGEZA  WIZARA YA KILIMO KWA KUPENDEKEZA   ASA   KATIKA UTEKELEZA WA PROGRAMU YA  TFSRP

Na Mwandishi wetu- Morogoro

Kaimu Mtendaji Mkuu wa Wakala wa  Mbegu za Kilimo (ASA) Bw. Leo Mavika ameipongeza  Wizara ya Kilimo kwa kuipendekeza (ASA) katika utekelezaji wa Programu ya Mifumo Himilivu ya Chakula Tanzania (TFSRP) .

Shukrani hizo  zimetolewa  Septemba 13, 2025 na Bw. Mavika wakati akifunga mafunzo  ya  Matumizi sahihi ya Viuwatilifu  na utunzaji  wa Mazingira kupitia  Program ya Mifumo himilivu ya Chakula Tanzania  (TFSRP). 

Bw. Mavika amesema, mafunzo hayo ni muhimu kwetu ili kuongeza uzalishaji  wenye tija na kutunza mazingira. 

"Mafunzo haya yatawajengea uwezo wa kufanya Matumizi sahihi ya Viuwatilifu  na utunzaji  wa Mazingira mashambani, hii itachochea mazingira rafiki ya uzalishaji wa mbegu bora za kilimo na tija" amesema Bw. Mavika

“Naishukuru  Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya Rais wa awamu ya sita Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kutoa fedha kwa ajili ya Sekta ya Kilimo” amesema Bw. Mavika

Aidha  amempongeza  Waziri wa Kilimo Mhe. Hussein Bashe (Mb) na Menejimenti ya Wizara ya kilimo kwa kuipambania Sekta ya kilimo na kuleta mageuzi makubwa ya Kilimo hapa nchini kwa kusimamia vema upatikanaji wa fedha kwa ajili ya programu hii na shughuli mbalimbali za kilimo ikiwa  ni pamoja na  kuipendekeza ASA katika utekelezaji wa  Mradi huu wa TFSRP.