ASA YAZINDUA RASMI KAMATI YA UKAGUZI
24 Oct, 2025
ASA YAZINDUA RASMI KAMATI YA UKAGUZI

Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Mbegu za Kilimo (ASA) Bw. Leo Martin  Mavika amezindua kamati ya ukaguzi mapema leo Oktoba 24 mwaka 2025 katika ukumbi wa Vikao Makao makuu ya Wakala wa Mbegu za Kilimo( ASA) Mkoani Morogoro.

Bw, Leo Mavika ameitaka  kamati hiyo kufanya kazi Vizuri huku akiihakikishia ushirikiano wa kutosha kutoka kwa Wajumbe wa Menejimenti ili malengo ya Taasisi  yatimie kwa wakati.

Aidha katika uzinduzi huo Mwenyekiti wa Kamati hiyo CPA Daniel  John  Mark  aliongoza kikao hicho kwa kujadili taarifa mbalimbali ikiwemo nyaraka za Kamati ya Ukaguzi ambazo ni audit committee charter na Mpango kazi , Nyaraka za kitengo cha ukaguzi wa ndani ambazo ni internal audit charter, Mpango mkakati wa miaka mitatu (strategic internal audit plan) ya miaka 2025/26 mpaka 2027/28, Mpango kazi wa mwaka (risk based internal audit plan) wa mwaka 2025/26, pamoja na taarifa ya ukaguzi wa ndani wa robo ya kwanza kwa mwaka wa fedha 2025/26.