ASA YAENDELEA KUSOGEZA HUDUMA YA UPATIKANAJI WA MBEGU BORA ZA KILIMO KWA WAKULIMA KATIKA MAONESHO YA KILIMO YA SAMIA KILIMO BIASHARA EXPRO 2025, GAIRO.
03 Oct, 2025
ASA YAENDELEA KUSOGEZA HUDUMA YA UPATIKANAJI WA MBEGU BORA ZA KILIMO KWA WAKULIMA KATIKA MAONESHO YA KILIMO YA  SAMIA KILIMO BIASHARA EXPRO  2025, GAIRO.

Wakala wa Mbegu za kilimo (ASA), imesogeza huduma yake ya upatikanaji wa  mbegu bora za kilimo  katika maonesho ya nne ya SAMIA KILIMO BIASHARA yanayofanyika wilaya ya Gairo mkoani Morogoro.

Baadhi ya wakulima katika wilaya ya Gairo mkoani Morogoro wamefurahishwa na huduma hii na upatikanaji wa mbegu  bora za kilimo karibu yao kutoka ASA, baada ya kupatiwa elimu ya namna bora ya matumizi ya mbegu zilizothibitishwa ili kuongeza uzalisha wenye tija kwa wakulima nchini.

Mbegu hizo ambazo huvumilia hali ya ukame na kutobunguliwa na wadudu, zimewafanya wakulima hao kuendelea kuchangamkia fursa hiyo na kujipatia mbegu bora hizo ili kuzalisha mazao hayo kwa wingi.

Pia, Mkuu wa Wilaya ya Makete Mhe. Kissa Kasongwa, ameipongeza ASA kusogeza huduma ya upatikanaji wa mbegu bora za kilimo kwa wakulima na kuwapa elimu ya matumizi sahihi ya mbegu kwani elimu hiyo itaongeza kipato kwa mkulima na kumwinua kiuchumi. 

Wakala wa mbegu za kilimo (ASA), wanashiriki katika maonesho ya Samia Kilimo Expo katika wilaya ya Gairo ikiwa ni msimu wa nne.